Jeremiah 50:3-8


3 aTaifa kutoka kaskazini litamshambulia,
na kuifanya nchi yake ukiwa.
Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake,
watu na wanyama wataikimbia.


4 b“Katika siku hizo, wakati huo,”
asema Bwana,
“watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda
wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mwenyezi Mungu wao.

5 cWataiuliza njia iendayo Sayuni
na kuelekeza nyuso zao huko.
Watakuja na kuambatana na Bwana
katika agano la milele
ambalo halitasahaulika.


6 d“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea;
wachungaji wao wamewapotosha
na kuwasababisha kuzurura
juu ya milima.
Walitangatanga juu ya mlima na kilima,
na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.

7 eYeyote aliyewakuta aliwala;
adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia,
kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi,
Bwana, aliye tumaini la baba zao.’


8 f“Kimbieni kutoka Babeli;
ondokeni katika nchi ya Wakaldayo
tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
Copyright information for SwhKC